FIFA inatarajiwa kuthibitisha muundo mpya wa Kombe la Dunia la 2026, na kupanua mashindano hayo hadi michezo 104 kwa muda wa siku 39.
Uamuzi huo utaidhinishwa katika kikao cha Baraza la FIFA leo Jumanne katika mji mkuu wa Rwanda Kigali, ambapo wakuu wa soka duniani wamekusanyika kwa ajili ya kongamano la kila mwaka siku ya Alhamisi
Ikiandaliwa na Kanada, Mexico na Marekani, toleo la 2026 tayari litakuwa Kombe kubwa zaidi la Dunia, lenye timu 48 na litachezwa kwa muda mrefu zaidi
Wazo la awali lilikuwa kuwa na makundi 16 ya timu tatu tatu, mchujo kufanyika kupata timu 32, timu mbili kutoka kundi
Mpangilio huo ungehusisha michezo 80, kutoka kwa mfumo wa michezo 64 ambao FIFA imetumia tangu 1998.
Lakini kuwa na timu tatu kwenye kundi inaweza kupoteza msisimko wa raundi ya mwisho ya michezo ya hatua ya makundi kwa wakati mmoja, na pia inaongeza nafasi ya timu hizo mbili katika mchezo uliopita kushirikiana ili kuandaa matokeo wanayohitaji



