Kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa wiki raundi ya nne ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Chama ametwaa tuzo hiyo baada ya kupigiwa kura kwa wingi akiwashinda Peter Shalulile wa Mamelodi Sundowns, Ahmed Zizo wa Zamalek na Walid Sabbar wa Raja Casablanca
Chama ameibuka mshindi kwa kupata kura zaidi ya asilimia 68 ya kura zote zilizopigwa
Kiungo huyo mahiri pia amejumuishwa kwenye kikosi bora cha wiki pamoja na mchezaji mwingine wa Simba Shomari Kapombe
Chama alifunga bao pekee la Simba kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Vipers Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa March 07 na Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0




