Chama mchezaji bora wa wiki CAF CL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th March 2023


Chama mchezaji bora wa wiki CAF CL

Kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa wiki raundi ya nne ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Chama ametwaa tuzo hiyo baada ya kupigiwa kura kwa wingi akiwashinda Peter Shalulile wa Mamelodi Sundowns, Ahmed Zizo wa Zamalek na Walid Sabbar wa Raja Casablanca

Chama ameibuka mshindi kwa kupata kura zaidi ya asilimia 68 ya kura zote zilizopigwa

Kiungo huyo mahiri pia amejumuishwa kwenye kikosi bora cha wiki pamoja na mchezaji mwingine wa Simba Shomari Kapombe

Chama alifunga bao pekee la Simba kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Vipers Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa March 07 na Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.