Gianni Infantino amechaguliwa kwa mara nyingine kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kwenye uchaguzi uliofanyika leo jijini Kigali Rwanda
Katika uchaguzi huo Infantino alikuwa mgombea pekee na ataongoza chombo hicho kikubwa cha mpira duniani mpaka 2027
"Ni heshma na fahari kwangu kuchaguliwa tena kama Rais wa FIFA," alisema Infantino baada ya kutangazwa
Infantino alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuwa Rais wa FIFA mwaka 2016 kufuatia kujiuzulu kwa mtangulizi wake Sepp Blatter, na kushika wadhifa wake bila kupingwa miaka mitatu baadaye.
Lakini hii inahesabiwa kuwa muhula wake wa pili wa ofisi na kwa hivyo anaweza kugombea tena muhula wa tatu na wa mwisho katika muda wa miaka minne



