Mshambulizi wa kati wa Ivory Coast Sebastien Haller ameitwa kwenye kikosi cha taifa kwa mechi dhidi ya Comoro siku ya Jumatano baada ya kukosekana kwa miezi kadhaa ambapo alipatiwa matibabu ya saratani ya tezi dume
Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 28 alijiunga na Borussia Dortmund mwezi Julai kutoka Ajax na baadae kugundulika ana saratani
Alifanyiwa upasuaji mara mbili na mizunguko minne ya chemotherapy kabla ya kuanza tena mazoezi mwezi Januari. Alianza kucheza tena Januari 22 na kufunga bao lake la kwanza baada ya kuugua Februari 4 dhidi ya Freiburg
Haller, ambaye amefunga mabao manne akiichezea timu ya taifa ya Ivory Coast, atacheza mechi dhidi ya Comoro Machi 24 na 28 kama sehemu ya kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika 2023.
Winga wa Lille Jonathan Bamba pia ameitwa kwa mara ya kwanza akiwa ameichezea Ufaransa katika ngazi ya vijana.
Ivory Coast ndio wenyeji wa michuano hiyo ambayo imerudishwa nyuma kuanzia Juni na Julai hadi Januari-Februari 2024 ili kuepuka msimu wa mvua



