Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa March 17 2023

Joel JJ By Joel JJ
17 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa March 17 2023

Manchester United wako tayari kuwasilisha dau la kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham, 19, kutoka Borussia Dortmund. (Telegraph - usajili unahitajika)

Newcastle United wanataka kumpa kipaumbele kiungo wa Leicester James Maddison msimu huu wa joto huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 akisemekana kutaka kucheza Ligi ya Mabingwa na kuwa mchezaji wa kawaida katika kikosi cha England. (The I)

Muda wa mkopo wa Dele Alli katika klabu ya Besiktas hautafanywa kuwa wa kudumu msimu wa joto, huku Everton wakitarajiwa kusitisha kandarasi ya kiungo huyo Mwingereza mwenye umri wa miaka 26. (Football Insider)

Thierry Henry amekataa nafasi ya kuwa kocha mkuu wa timu ya wanawake ya Ufaransa. (Le Figaro - kwa Kifaransa)

Klabu za Manchester United, Newcastle, Brighton na Brentford zimeonyesha nia ya kumnunua kiungo wa kati wa Uhispania na Celta Vigo Gabri Veiga pamoja na vilabu vingine vya Premier League pia hapo awali vilivyoonyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (90 Min)

Winga wa Brighton Solly March, 28, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo wakati mkataba wake wa sasa ukitarajiwa kumalizika msimu huu wa joto. (The Athletic)

Wolves wako tayari kumpa mkataba mpya nahodha na kiungo wa kati wa Ureno Ruben Neves, 26. (90 Min)

Bayer Leverkusen wana nia ya kumsajili beki wa West Ham na Jamhuri ya Czech Vladimir Coufal, 30. (Football Insider)

Crystal Palace watafanya uamuzi kuhusu mustakabali wa meneja Patrick Vieira wakati wa mapumziko ya kimataifa. (Telegraph - usajili unahitajika)

Beki wa zamani wa Tottenham na England Danny Rose, 32, anafanya mazoezi na klabu ya York City inayoshiriki Ligi ya Taifa, akiwa hana klabu tangu mkataba wake wa Watford ulipokatizwa mwezi Septemba. (Sun)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
6h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
7h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
9h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
9h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
10h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
10h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
11h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
11h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
11h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
13h ago
READ MORE →