Klopp akiri mambo magumu Liverpool

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th March 2023


Klopp akiri mambo magumu Liverpool

Mkufunzi wa Livepool Jurgen Klopp anasema wanakabiliwa na kazi kubwa kurejea katika Ligi ya Mabingwa baada ya kipigo cha Real Madrid

Majogoo hao walibomolewa 5-2 dimba la Anfield wiki tatu zilizopita na bao la dakika za lala salama la Karim Benzema kwenye Uwanja wa Bernabeu likafanya kushindwa kwa Liverpool kwa jumla ya mabao 6-2

Dalili sio nzuri kwa upande wao kwani wanahatari ya kutoshiriki ligi ya mabingwa msimu ujao kama fomu yao haitaimarika. Wanashika nafasi ya sita kwenye msimamo wa Premia alama sita nyuma ya Tottenham inayoshika nafasi ya nne

"Tulijiandaa kupambana lakini hatukuweza kupata matokeo tuliyoyahitaji uwanjani. Ilikuwa dhahiri, mpango wetu uliharibika tangu mchezo wa kwanza" alisema Klopp.

Nyota watatu ambao walikuwa na mchango mkubwa kuipeleka Liverpool kwenye fainali tatu za Ligi ya Mabingwa ndani ya miaka mitano, Sadio Mane aliondoka kwenda Bayern Munich msimu uliopita wa joto, Roberto Firmino anaondoka mwishoni mwa msimu huu huku Mohamed Salah akishindwa kufikia ubora ambao wengi walimuona katika misimu iliyopita

Nahodha Jordan Henderson anatimiza miaka 33 mwishoni mwa msimu na James Milner, aliyeanza Bernabeu, ana miaka 37

Kiungo wa zamani wa Scotland, Charlie Adam, ambaye aliichezea Liverpool 2011-12, alisema Klopp anahitaji kukiongezea nguvu kikosi chake

"Nadhani Jurgen Klopp amekuwa mwaminifu sana kwa wachezaji hawa, lakini nadhani anahitaji nguvu mpya kwenye kikosi chake"


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.