Klabu ya Horoya Ac ya Guinea na US Monastir ya Tunisia zimewasili nchini Alfajiri ya leo Ijumaa kuelekea mechi za michuano ya CAF dhidi ya Simba na Yanga
Kesho Jumamosi Horoya Ac watakuwa wageni wa Simba katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika
Simba inahitaji kushinda mchezo huo utakaopigwa saa 1 usiku ili kutinga robo fainali kwa mara ya tatu katika kipindi cha miaka mitano iliyopita

US Monastir wao watakuwa wageni wa Yanga katika mchezo wa kombe la Shirikisho ambao utapigwa Jumapili katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Mazingira ya mchezo huo hayatofautiana na ule wa Simba kwani Yanga inahitaji kushinda ili kutinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika
Baada ya kushiriki hatua ya makundi ymara mbili pasipo mafanikio, hii ni nafasi adimu kwa Yanga kutinga robo fainali kwa mara ya kwanza katika michuano hiyo
Mchezo huo pia utapigwa saa 1 usiku



