Hersi awaongoza mashabiki wa Yanga kuchangia damu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th March 2023


Hersi awaongoza mashabiki wa Yanga kuchangia damu

Rais wa klabu ya Yanga Injinia Hersi Said leo amewaongoza wapenzi, wanachama na mashabiki wa Yanga katika zoezi la kuchangia Damu linaloendelea Makao Makuu ya klabu hiyo na Hospitali ya Mloganzila, jijini Dar es salaam

Yanga kwa kushirikiana na mpango wa Taifa wa damu salama Hospitali ya Mloganzila pamoja na Hospitali ya Mifupa MOI, waliandaa zoezi la uchangiaji damu kwa ajili ya kuimarisha benki ya damu kuwasaidia wagonjwa wenye mahitaji ya kuongezewa damu

Kwa wote wanaojitokeza kuchangia damu, Yanga inatoa zawadi ya jezi na tiketi kwa ajili ya kushuhudia mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya US Monastir ambao utapigwa Jumapili, March 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.