Rais wa klabu ya Yanga Injinia Hersi Said leo amewaongoza wapenzi, wanachama na mashabiki wa Yanga katika zoezi la kuchangia Damu linaloendelea Makao Makuu ya klabu hiyo na Hospitali ya Mloganzila, jijini Dar es salaam
Yanga kwa kushirikiana na mpango wa Taifa wa damu salama Hospitali ya Mloganzila pamoja na Hospitali ya Mifupa MOI, waliandaa zoezi la uchangiaji damu kwa ajili ya kuimarisha benki ya damu kuwasaidia wagonjwa wenye mahitaji ya kuongezewa damu
Kwa wote wanaojitokeza kuchangia damu, Yanga inatoa zawadi ya jezi na tiketi kwa ajili ya kushuhudia mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya US Monastir ambao utapigwa Jumapili, March 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa







