Msafara wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' umeondoka leo kuelekea Misri kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu Afcon 2023 dhidi ya Uganda
Kikosi kilichoondoka leo hakijumuishi wachezaji wa Yanga ambao wataondoka baada ya mchezo wao wa kombe la Shirikisho dhidi ya US Monastir ambao utapigwa leo
Mechi ya kwanza dhidi ya Uganda itapigwa March 24 huko Misri na mchezo wa mrudiano kupigwa March 28 jijini Dar es salaam







