Baada ya kuwashuhudia watani zao Simba wakitinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kibabe kwa ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya Ac, leo ni zamu ya Wananchi Yanga ambao wanashiriki michuano ya kombe la Shirikisho
Yanga itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili US Monastir katika mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali
Yanga wanahitaji ushindi ili kutinga robo fainali kuweka rekodi yao mpya katika michuano hiyo
Hii ni mara ya tatu kwa Yanga kucheza hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho lakini mara mbili ilishindwa kupenya robo fainali
Msimu huu Yanga imeonyesha ubora na kwa hakika Wananchi watajilaumu wenyewe kama watashindwa kutinga robo fainali
Wanahitaji kukata tiketi yao mapema ili uondoa presha katika mchezo wa mwisho ambao watakuwa ugenini dhidi ya TP Mazembe
Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kiko tayari akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa leo kuishangilia timu yao