Tottenham

Conte awabwatukia wachezaji, mabosi Spurs

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Mar 2023
Conte awabwatukia wachezaji, mabosi Spurs

Meneja wa Tottenham, Antonio Conte, aliwalaumu wachezaji wake baada ya kutangulia kwa mabao mawili na kulazimishwa sare ya 3-3 dhidi ya Southampton, akihoji vikali motisha yao na malengo ya klabu

Muitaliano huyo, anayetarajiwa kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu, pia alitia shaka mustakabali wake kwa kumkosoa mmiliki, Joe Lewis, na mwenyekiti wa klabu, Daniel Levy.

"Kwangu mimi hii haikubaliki," Conte alisema, James Ward-Prowse baada ya kufunga penalti kukamilisha kurejea kwa Saints katika sekunde za mwisho. Tunaongoza 3-1, lakini tunaruhusu kufungwa mabao mawili kirahisi"

Conte, akijibu maswali mawili tu katika dakika 10, alienda mbali zaidi kulaumu sare hiyo ambayo iliharibu matumaini ya Tottenham kumaliza kwenye top four

"Nadhani ni bora kuingia kwenye shida, sisi sio timu, Sisi ni wachezaji 11 wanaoingia uwanjani. Ninaona wachezaji wenye ubinafsi, wachezaji ambao hawataki kusaidiana na wasioweka moyo wao kwenye timu. Msimu huu ikilinganishwa na uliopita, tumefanya vibaya sana"

"Imekuwa hivi kwa miaka 20 sasa tunacheza tu kujifurahisha, haishangazi kuona timu haijashinda taji lolote katika kipindi hicho. Hakuna dhamira ya dhati ya kubadilisha hali hii," alisema Conte

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’