Wachezaji nane waliochelewa kujiunga na timu ya Taifa huko Misri kutokana na sababu mbalimbali, wamewasili nchini humo kuungana na wenzao kuelekea mchezo dhidi ya Uganda
Msafara uliotua usiku wa kuamkia leo umejumuisha wachezaji saba wa Yanga na Mzamiru Yassin wa Simba naliyekuwa na ruhusa maalum
Nyota wa Yanga waliotua ni Metacha Mnata, Kibwana Shomari, Dickson Job, Bakari Nondo Mwamnyeto, Ibrahim Bacca, Mudathir Yahya na Feisal Salum





