Simba

Simba yapiga hesabu ya nusu fainali Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Mar 2023
Simba yapiga hesabu ya nusu fainali Ligi ya Mabingwa

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba, Salum Abdallah 'Try Again' amesema kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ni moja ya malengo yao na kusisitiza wanaelekea kufikia hatua waliyokuwa wanaitamani miaka mingi yaani nusu fainali

Simba imetinga robo fainali kibabe baada ya kuifunga Horoya ya Guinea kwa mabao 7-0 ikifikisha pointi tisa ikiwa nyuma ya Raja Casablanca iliyokusanya pointi 13 ikiongoza Kundi C, Horoya ikiwa ya tatu na pointi nne na Vipers inaburuza mkia na pointi mbili kila timu ikicheza mechi tano.

Try Again amebainisha kuwa malengo ya klabu hiyo yalikuwa ni kuhakikisha wanaitengeneza Simba kuwa tishio ambayo inaweza kupambana na timu zingine kubwa zaidi Afrika sehemu ambayo ndio wanaelekea sasa

"Tulikuwa kwenye mtihani mkubwa wa kuhakikisha tunaiona Simba ikitinga hatua ya robo fainali hili limefanikiwa. Tulibezwa sana kwamba tuna kikosi kibovu, lakini safari inaendelea sasa na huko tuendako pia tuna nafasi ya kufanya vizuri pamoja na wengi kuzungumza mambo mengi"

"Tutawajibu kwa vitendo mpira unachezwa uwanjani na sio midomoni mwa watu kama ingekuwa hivyo kwa kuzungumzwa Simba inafungwa tusingeweza kufika hapa tulipo sasa tusubiri dakika nyingine tutakazozipata matokeo ndio yataamuliwa na tupo tayari kupambana na yeyote." alisema Try Again.

"Licha ya kupenya robo fainali, mikakati yatu ni kuifanya Simba kuwa kwenye ushindani na timu kama Raja Casablanca iliyotuonyesha ubora na tumejifunza kitu kutoka kwao na vile tuna mchezo dhidi yao kukamilisha ratiba tutaendelea kwenda kupambana na kujifunza ili kujipanga kwa robo fainali"

"Tunataka kuwa na timu bora na ya ushindani yenye kutamba Afrika na nje ya mipaka ya bara hili. Hapa tulipo ni mwanzo tena wa mbali sana katika kusuka klabu ambayo haitakuwa na mpinzani wa kushindana nayo," aliongeza Try Again.

Simba itasafiri Morocco kumalizia mechi ya makundi itakayopigwa Aprili 1 dhidi ya Raja Casablanca ambao waliwafunga mabao 3-0 nyumbani

Katika hatua ya robo fainali, Simba inaweza kukutana na Mamelodi, Esperance au Wydad Casablanca ambazo zinaonekana kuwa nafasi nzuri ya kumaliza vinara wa makundi yao

Mwanaspoti

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’