PSG

Mbappe nahodha Ufaransa

Joel JJ By Joel JJ
21 Mar 2023
Mbappe nahodha Ufaransa

Kylian Mbappe atachukua nafasi ya nahodha wa Ufaransa baada ya Hugo Lloris kujiuzulu kufuatia kushindwa kwa fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina, chanzo cha karibu cha timu hiyo kimeiambia AFP.

Mshambulizi wa Paris Saint-Germain Mbappe, 24, amekubali jukumu hilo baada ya mazungumzo na kocha Didier Deschamps

Mchezo wake wa kwanza kama nahodha utakuwa wa Ijumaa wa kufuzu kwa Euro 2024 dhidi ya Uholanzi Uwanja wa Stade de France

Itakuwa mechi ya kwanza ya Les Bleus tangu kushindwa kwenye fainali ya Kombe la Dunia huko Doha mnamo Desemba 18.

Kipa wa Tottenham Lloris, 36, alimaliza soka lake la kimataifa mwezi Januari, wiki chache baada ya Argentina kuwashinda Wafaransa hao kwa mikwaju ya penalti kufuatia mechi ya kusisimua iliyoisha 3-3 katika muda wa ziada.

Lloris alikuwa nahodha kwa zaidi ya muongo mmoja. Mshambulizi wa Atletico Madrid Antoine Griezmann alitangazwa kuwa makamu wa nahodha baada ya beki wa kati wa Manchester United Raphael Varane pia kutundika daruga zake kufuatia kushindwa na Argentina mwezi Desemba.

Mbappe, ambaye alifunga hat-trick kwenye fainali ya Kombe la Dunia, alikuwa akihusishwa pakubwa na nafasi ya unahodha kwa wiki kadhaa

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
3h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
6h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
6h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
7h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
7h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
7h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
7h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
8h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →