Wachezaji wawili wa Simba Clatous Chama na Sadio Kanoute wameorodheshwa katika kinyan'ganyiro cha kuwania tuzo ya mchezaji bora wa wiki Ligi ya Mabingwa barani Afrika
Chama alifunga hat-trik katika mchezo wa raundi ya tano dhidi ya Horoya Ac huku kanoute akifunga mabao mawili
Wanachuana na Mahmoud Karhaba wa Al Ahly ambaye pia alifunga hat-trik katika mchezo dhidi ya Cotton Sport na Pecy Tau wa Al Ahly pia aliyefunga bao moja na kutoa pasi mbili za mabao katika mchezo huo
Chama alishinda tuzo hiyo katika mzunguuko wa nne na huenda akashinda tena kwa mara ya pili mfululizo
Kura zinapigwa kupitia ukurasa wa Twitter wa CAF CL

Katika kikosi cha wiki cha CAF, Simba imeingiza wachezaji wanne Jean Baleke na Shomari Kapombe wakiungana na Chama na Kanoute