Stars matumaini kibao kuelekea mchezo dhidi ya Uganda Cranes

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd March 2023


Stars matumaini kibao kuelekea mchezo dhidi ya Uganda Cranes

Kocha Msaidizi wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Hemed Morocco, amesema maandalizi yanaendelea vizuri na wanamatumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mchezo wa kutasaka nafasi ya kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2023 dhidi ya Uganda siku ya Ijumaa

Morocco amesema maandalizi yako vizuri baada ya kufanya mazoezi ya gym ya kutafuta stamina na uwanjani, wachezaji watakuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo.

Alisema wachezaji wameanza kuelewana licha ya kukutana muda mfupi, wanaimani nao kupambana katika mchezo huo ili kupata matokeo mazuri .

"Tunatambua mechi itakuwa ya ushindani mkubwa kwa sababu ya ugumu wa mchezo hasa tunapokutana na Uganda, ni imani yangu kwa wachezaji tuliokuwa nao tutapata matokeo mazuri," alisema kocha huyo.

Alisema wanaendelea kufanya mazoezi ya nguvu kuhakikisha wanapata matokeo katika mchezo huo ili kupata kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu.

Morocco alisema anatumai wanaweza kupata matokeo katika mcheo huo na ule wa marudianoa utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam Jumanne ijayo.

Katika msimamo wa Kundi F, Algeria ipo kileleni ikiwa na pointi sita ikifuatiwa na Niger yenye alama mbili huku Taifa Stars na Uganda zikifuata kutokana na kulingana kila kitu kila moja akiwa na pointi moja.

Timu mbili zitakazoshika nafasi ya juu kutoka katika kila kundi zitafuzu kushiriki michuano hiyo ya Afcon itakayofanyika nchini Ivory Coast baadaye mwaka huu.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.