Tanzania - Taifa Stars - Yanga - Simba - Azam

Tanzania kuikabili Uganda kufuzu Afcon 2023 leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Mar 2023
Tanzania kuikabili Uganda kufuzu Afcon 2023 leo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo majira ya saa 11 itashuka dimba la Suez Canal huko Ismailia, Misri kuikabili Uganda Cranes katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2023

Uganda ndio wenyeji wa mchezo huo ambao walilazimika kuupeleka Misri baada ya CAF kukataa viwanja vya Uganda kwa kukosa sifa

Hii ni nafasi ya adimu kwa Tanzania kusaka ushindi katika mchezo ambao ni kama timu zote zitakuwa ugenini

Baada ya Niger kuchapwa mabao 2-1 na Algeria hapo jana, timu itakayoshinda leo itapanda mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi F

Itakuwa mechi ya kwanza kwa kocha Adel Amrouche ambaye alikabidhiwa majukumu ya kuinoa Stars hivi karibuni

Amrouche amesema pamoja na vijana wake kupata muda mfupi wa kufanya mazoezi ya pamoja, wako tayari kwa mchezo huo ambao dhamira yao ni kusaka ushindi

Mchezo wa marudiano utapigwa jijini Dar es salaam siku ya Jumanne, March 28 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’