Bayern yamfuta kazi Nagelsmann

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th March 2023


Bayern yamfuta kazi Nagelsmann

Mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wamemfuta kazi Kocha wao Mkuu Julian Nagelsmann

Uamuzi huo umechukuliwa mara moja huku ikibainishwa kuwa wakati wowote watamtangaza kocha wa zamani wa Chelsea Thomas Tuchel kuwa mrithi wake

Tuchel anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuwanoa matajiri hao wa Ujerumani

Msimu huu Bayern wamekuwa na mwenendo wa kusuasua kwenye ligi wakishika nafasi ya pili nyuma ya Borussia Dortmund wakizidiwa alama moja

Hata hivyo Nagelsmann aliiwezesha Bayern kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya kwa kuwaondosha PSG kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-0

Baada ya kutimuliwa na Beyern, Nagelsmann anaweza kuibukia Uingereza kunako klabu ya Tottenham Hotspurs ambayo inatarajiwa kumfuta kazi Antonio Conte


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.