Messi afikisha mabao 800

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th March 2023


Messi afikisha mabao 800

Nyota wa Argentina aliyeshinda Kombe la Dunia, Lionel Messi aliliongoza Taifa lake kuifunga Panama 2-0 siku ya Alhamisi katika mechi ya kirafiki ambayo kimsingi ilikuwa kusherehekea ushindi wao wa Kombe la Dunia Desemba mwaka jana

Mabingwa hao wa dunia walitawala mchezo huo, hawakupata bao hadi dakika ya 78 pale Thiago Almada alipofunga bao baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Messi kugonga nguzo ya goli

Dakika kumi baadae, ilikuwa zamu ya Messi na akafunga bao la 800 la taaluma yake kwa mkwaju wa faulo. Sasa amefunga mabao 99 kwenye timu ya Taifa ya Argentina

Messi anakuwa mchezaji wa pili kuwahi kufikisha mabao 800 nyuma ya Ronaldo ambaye anashikilia rekodi ya muda wote ya kufunga mabao 830


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.