Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi Simba, Salim Abdalah 'Try Again' amedokeza dhamira wa nahodha wa timu hiyo John Bocco kugeukia katika ukocha
Try Again aliyasema hayo mapema jana wakati Simba ikisaini mkataba wa miaka miwili na kampuni ya Mobi Ad kwa ajili ya kuendeleza na kukuza soka la vijana
Try Again alibainisha kuwa Bocco mara kadhaa amekuwa akimwambia juu ya ndoto yake ya kuwa kocha na sasa njia kwake ni nyeupe kutokana na uwekezaji ambao umeanza kufanywa kwa vijana katika klabu ya Simba
"Bocco nahodha wetu na wewe ndoto yako ya kuwa kocha wa vijana inatimia sasa maana mara kwa mara umekuwa ukiniambia kuhusu hilo, hivi karibuni tutaanza ujenzi wa akademi yetu na tayari niliongea na mwekezaji wetu," alisemaTry Again
Bocco amekuwa sehemu ya kikosi cha Simba kwa misimu sita akiisaidia Simba kutwaa ubingwa wa ligi kuu mara nne mfululizo
Pia Simba ikishinda Ngao ya Jamii mara tatu na kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) huku ikicheza robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa mara tatu na kombe la Shirikisho mara moja
Kabla ya kujiunga na Simba, Bocco aliitumikia Azam Fc kwa takribani misimu 10 akishiriki kuipandisha timu hiyo Ligi Kuu pamoja na kuisaidia kutwaa ubingwa wa ligi kuu pekee msimu wa 2013/14



