Chelsea - Inter - Ac Milan

Lukaku aizamisha Sweden kufuzu Euro 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Mar 2023
Lukaku aizamisha Sweden kufuzu Euro 2024

Mshambuliaji wa Chelsea ambaye anaitumikia Inter Milan kwa mkopo, Romelu Lukaku jana alifunga hat-trick na kuiongoza Ubelgiji kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Uswidi katika mechi ya kufuzu kwa Euro 2024

Yawezekana wengi wamepoteza imani kwa mshambuliaji huyu mwenye asili ya DR Congo, lakini anapokuwa kwenye majukumu ya timu yake ya Taifa, huwa ni tofauti

Ulikuwa ushindi muhimu kwa Ubelgiji waliopata ugenini katika mchezo ambao pia alishuhudiwa mshambuliaji mkongwe Zlatan Ibrahimovic akiterejea kuitumikia Sweden baada ya mwaka mmoja

Ibrahimovic, 41, aliingia dakika ya 73 kwa shangwe kutoka kwa mashabiki wa Uswidi. Ilikuwa ni mechi yake ya kwanza ya kimataifa baada ya kutangaza kustaafu mwaka uliopita.

Akiwa na umri wa miaka 41, miezi mitano na siku 21, Ibrahimovic alitajwa kuwa amevunja iliyokuwa ikishikiliwa na kipa wa Italia Dino Zoff tangu 1983, kama mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kucheza mechi ya kufuzu michuano ya Ulaya.

Hata hivyo, mshambuliaji wa Gibraltar Lee Casciaro - ambaye ana umri wa siku nne zaidi ya Ibrahimovic - aliweka rekodi katika mechi ya timu yake kushindwa 3-0 nyumbani na Ugiriki katika Kundi B Ijumaa.

Wikiendi iliyopita, Ibrahimovic alikuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kufunga bao katika historia ya Serie A wakati mshambuliaji huyo wa AC Milan alipofunga penalti dhidi ya Udinese.

Ibrahimovic amesema anataka kucheza Euro 2024 nchini Ujerumani mwaka ujao atakapofikisha umri wa miaka 42, na atakuwa mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kushiriki michuano hiyo

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
32m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
44m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’