Ufaransa iliibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Uholanzi mbele ya mashabiki 75,000 wenye furaha katika uwanja wa Stade de France Ijumaa usiku katika mchezo wa kuwania kufuzu Euro 2024
Ulikuwa mchezo wa kwanza kwa winga Kylian Mbappe (24) kuiongoza Ufaransa baada ya kuteuliwa kuwa nahodha na Didier Deschamps
Hakuna maneno ambayo yanaweza kuelezea umahiri wa miguu ya winga huyo wa PSG
Deschamps aliamiani Mbappe anatosha kujaza viatu vilivyoachwa na mlinda mlango Hugo Lloris, ambaye alishikilia nafasi hiyo kwa miaka 14
Mbappe anatabiriwa kufanya zaidi ya hapo, anaweza kuwa mchezaji bora zaidi ulimwenguni
Bao lake la kwanza kama mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa lilifunga dhidi ya Uholanzi kwenye Uwanja wa Stade de France karibu miaka sita iliyopita, na akaendeleza ubabe wake dhidi ya Uholanzi akiibuka kuwa mchezaji bora wa mechi
Mabao yake mawili yalihitimisha ushindi huo muhimu nyumbani huku mabao mengine yakifungwa na Antoine Griezmann na Dayot Upamecano
Mbappe amefikisha mabao 37 katika timu ya Taifa ya Ufaransa akishika nafasi ya tano katika vinara wa ufungaji wa muda wote



