Mbappe apiga mbili Ufaransa ikiichapa Uholanzi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th March 2023


Mbappe apiga mbili Ufaransa ikiichapa Uholanzi

Ufaransa iliibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Uholanzi mbele ya mashabiki 75,000 wenye furaha katika uwanja wa Stade de France Ijumaa usiku katika mchezo wa kuwania kufuzu Euro 2024

Ulikuwa mchezo wa kwanza kwa winga Kylian Mbappe (24) kuiongoza Ufaransa baada ya kuteuliwa kuwa nahodha na Didier Deschamps

Hakuna maneno ambayo yanaweza kuelezea umahiri wa miguu ya winga huyo wa PSG

Deschamps aliamiani Mbappe anatosha kujaza viatu vilivyoachwa na mlinda mlango Hugo Lloris, ambaye alishikilia nafasi hiyo kwa miaka 14

Mbappe anatabiriwa kufanya zaidi ya hapo, anaweza kuwa mchezaji bora zaidi ulimwenguni

Bao lake la kwanza kama mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa lilifunga dhidi ya Uholanzi kwenye Uwanja wa Stade de France karibu miaka sita iliyopita, na akaendeleza ubabe wake dhidi ya Uholanzi akiibuka kuwa mchezaji bora wa mechi

Mabao yake mawili yalihitimisha ushindi huo muhimu nyumbani huku mabao mengine yakifungwa na Antoine Griezmann na Dayot Upamecano

Mbappe amefikisha mabao 37 katika timu ya Taifa ya Ufaransa akishika nafasi ya tano katika vinara wa ufungaji wa muda wote


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.