Yanga

Yanga yafukuzia rekodi ya kushinda mataji manne

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 Mar 2023
Yanga yafukuzia rekodi ya kushinda mataji manne

Kwa sasa mashabiki wa Yanga wana raha ya aina yake baada ya kuishuhudia timu yao ikitinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika

Wananchi wanaona kabisa ni msimu ambao huenda wakaenda kushuhudia kupatikana mafanikio makubwa katika klabu yao kwenye miaka ya hivi karibuni

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema baada ya kufanikiwa kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho, malengo sasa ni kuitafuta nusu fainali, fainali na hata kusaka taji la kwanza barani Afrika kwani inawezekana

Wakati bendera ya Kimataifa ikiendelea kupepea vyema, Yanga pia imedhamiria kutetea mataji yake yote ya ndani

Ngao ya Jamii tayari iko mikononi, dalili njema zinaonekana kwenye ligi kuu, Yanga ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama nane huku zikiwa zimesalia mechi sita kuhitimisha msimu

Kimahesabu Yanga inahitaji kushinda mechi tatu zinazofuata ili kutetea ubingwa. Kama Wananchi watashinda mehci dhidi ya Kagera Sugar, Simba na Singida Big Stars basi hesabu zitakamilika mapema tu

Lakini iwapo itatokea watani zao Simba watashindwa kupata ushindi katika mechi zao zinazofuata kazi itakuwa rahisi zaidi

Kwenye kombe la FA Wananchi wako hatua ya robo fainali wakitarajiwa kuchuana na Geita Gold

Kama hesabu zitakwenda sawa, Yanga inaweza kufunga msimu ikiwa na mataji manne na kufanya msimu huu kuingia katika kumbukumbu ya klabu

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
30m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
42m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’