Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amefichua kubadili mfumo wa uchezaji wa kikosi chake akiamini mfumo huo mpya unawawezesha kufunga mabao mengi
Wiki iliyopita Robertinho aliiongoza Simba kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya Ac
"Nafurahi muitikio wa wachezaji katika mfumo mpya wa uchezaji ni mzuri. Tumekuwa tukitengeneza nafasi nyingi lakini hapo awali tulikuwa hatufungi mabao mengi. Lakini katika mechi tatu zilizopita tumefanya vizuri"
"Tuna wachezaji wazuri pembeni Kapombe na Zimbwe ambao tunawatumia katika kushambulia. Tunaweka washambuliaji wawili kuhakikisha tunatumia vyema mipira ya krosi wanazopiga"
"Ni muhimu sana kutumia nafasi tunazotengeneza uwanjani ili na uhakika wa kushinda mechi," alisema Robertinho
Katika michezo minne iliyopita, Simba ilipachika mabao 12 pasipo kuruhusu wapinzani kutikisa nyavu zao
Kikosi kimerejea mazoezini kuanza maandalizi ya mchezo wa kukamilisha ratiba hatua ya makundi ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca. Mchezo huo utapigwa April 01 huko Morocco



