Mfumo mpya umelipa Simba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th March 2023


Mfumo mpya umelipa Simba

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amefichua kubadili mfumo wa uchezaji wa kikosi chake akiamini mfumo huo mpya unawawezesha kufunga mabao mengi

Wiki iliyopita Robertinho aliiongoza Simba kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya Ac

"Nafurahi muitikio wa wachezaji katika mfumo mpya wa uchezaji ni mzuri. Tumekuwa tukitengeneza nafasi nyingi lakini hapo awali tulikuwa hatufungi mabao mengi. Lakini katika mechi tatu zilizopita tumefanya vizuri"

"Tuna wachezaji wazuri pembeni Kapombe na Zimbwe ambao tunawatumia katika kushambulia. Tunaweka washambuliaji wawili kuhakikisha tunatumia vyema mipira ya krosi wanazopiga"

"Ni muhimu sana kutumia nafasi tunazotengeneza uwanjani ili na uhakika wa kushinda mechi," alisema Robertinho

Katika michezo minne iliyopita, Simba ilipachika mabao 12 pasipo kuruhusu wapinzani kutikisa nyavu zao

Kikosi kimerejea mazoezini kuanza maandalizi ya mchezo wa kukamilisha ratiba hatua ya makundi ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca. Mchezo huo utapigwa April 01 huko Morocco


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.