Transfer

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu, March 27 2023

Joel JJ By Joel JJ
27 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya Jumatatu, March 27 2023

Manchester United wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Benfica na Ureno Goncalo Ramos, 21, ambaye ana kipengele cha kuondoka cha euro milioni 120 (£105.6m). (Record, via Goal)

Mshambulizi Evan Ferguson, 18, atakataa kuhamia Manchester United kwa sababu mchezaji huyo wa kimataifa wa Jamhuri ya Ireland anadhani kusalia Brighton kutakuwa bora zaidi kwa maendeleo yake. (Sun)

Wakati huo huo, Manchester United watamfikiria kipa wa Brentford Mhispania David Raya, 27, kama mbadala wa mtani wake David de Gea, 32, ambaye bado hajakubali kusaini mkataba mpya. (Give Me Sport)

Chelsea wako tayari kutoa euro milioni 100 kumnunua mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 24, wa Napoli. (Football Insider)

Chelsea wako kwenye mazungumzo na kiungo wa kati wa Ufaransa N'Golo Kante, 31, kuhusu kandarasi mpya ya miaka miwili, kukiwa na chaguo la mwaka zaidi Stamford Bridge. (Fabrizio Romano)

The Blues wamesikitishwa na meneja wa zamani, Mjerumani Thomas Tuchel, kwa kuweka hadharani nia yake ya kumchukua kocha wa kiwango cha juu wa Uingereza Anthony Barry kwenda Bayern Munich. (Telegraph)

Arsenal wataipatia kipaumbele jaribio lingine la kumsajili kiungo wa kati wa Brighton na Ecuador Moises Caicedo, 21, msimu wa joto. (Football transfers)

Aston Villa, Newcastle na Brighton wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Alex Oxlade-Chamberlain, 29, ambaye mkataba wake na Liverpool unamalizika mwishoni mwa msimu huu. (Mail)

Barcelona wamejiondoa katika mbio za kumsajili kiungo wa kati wa Ureno na Wolves Ruben Neves, 26, msimu huu. (Fichajes - kwa Kihispania)

Kiungo wa kati wa Uhispania Sergio Busquets, 34, bado hajakubali mkataba mpya na Barcelona na anaweza kuhamia Ligi Kuu ya Soka. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Chelsea na Arsenal watamenyana katika kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa kati wa Everton na Ubelgiji Amadou Onana, 21, baada ya kuanza vyema soka lake Goodison Park. (Fichajes - kwa Kihispania)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
12h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
13h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
15h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
15h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
16h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
16h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
17h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
17h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
17h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
19h ago
READ MORE →