Tanzania - Taifa Stars - Yanga - Simba - Azam

Micho akiri ana kazi mbele ya Stars

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Mar 2023
Micho akiri ana kazi mbele ya Stars

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Uganda Milutin Sredojevic 'Micho' amesema kikosi chake kipo katika kipindi cha mpito ambapo wanatengeneza timu imara kutoka kwa wachezaji wazoefu na kuwaingiza wachezaji vijana

Akizungumza katika mkutano na wanahabari mapema leo, Micho alisema kukutana na Tanzania yenye wachezaji kadhaa wanaocheza nje (Misri, Saudi Arabia, Ubelgiji) pamoja na wale wa Simba na Yanga kunafanya timu Taifa Stars kuwa timu imara.

"Lazima nikiri Tanzania na Uganda ziko mazingira tofauti kwa sasa. Tunacheza na timu ambayo ina wachezaji katika klabu ambazo zimefuzu robo fainali ya michuano ya ligi ya nabingwa na kombe la Shirikisho. Tunacheza na timu ambayo imepeleka wachezaji nchi kama Morocco, Misri, Saudi Arabia na barani Ulaya"

"Sisi tuko katika kipindi cha mpito. Tunajaribu kuingia damu changa kwenye timu yetu baada ya wachezaji wetu wengi ambao muda wao wa kuitumikia timu ya Taifa unamalizika"

"Hautakuwa mchezo mwepesi hata kidogo lakini sisi tumekuja hapa kupambana kusaka matokeo muhimu kutuweka hai matumaini yetu kwenye michuano ya Afcon," aisema Michu

Nae nahodha wa Uganda Emmanuel Okwi amesema wamepata mapokezi mazuri Tanzania, wako tayari kwa mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa kesho Jumanne dhamira yao ikiwa kuibuka na ushindi

Okwi amesema walipoteza mchezo wao wa nyumbani hivyo nao watapambana ili kuhakikisha wanashinda na kufufua matumaini ya kushiriki fainali za Afcon 2023

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’