Stars kazi moja dhidi ya Uganda leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th March 2023


Stars kazi moja dhidi ya Uganda leo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inatupa karata muhimu kuwania tiketi ya kufuzu michuano ya Afcon 2023 kwa kuikabili Uganda katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Mtananange huo wa dabi ya Afrika Mashariki, utapigwa kuanzia saa 2 usiku

Huu ni mchezo muhimu kwa Tanzania kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu michuano ya Afcon 2023 ambayo itafanyika baadae mwaka huu huko Ivory coast

Ushindi kwa Stars dhidi ya Uganda leo utawafanya wafikishe alama saba hivyo kuhitaji alama moja tu katika mechi mbili zitakazokuwa zimebaki dhidi ya Niger na Algeria ili kufuzu

Jana Niger ilichapwa bao 1-0 na Algeria na hivyo kuwahakikisha Algeria kuwa timu ya kwanza kufuzu kwa michuano hiyo baada ya kufikisha alama 12

Tanzania inashika nafasi ya pili ikiwa na alama nne, Niger ni wa tatu wakiwa na alama mbili wakati Uganda wanaburuza mkia wakiwa na alama moja katika kundi F

Stars inahitaji angalau alama nane tu kuweza kufuzu, alama tatu lazima zipatikane kwa Mkapa leo halafu kumaliza kazi hapohapo kwa Mkapa kwenye mchezo utakaofuata dhidi ya Niger mwezi Juni

Habari njema ni kuwa hakuna kiingilio kwa majukwaa ya Mzunguuko, mageti ya dimba la Mkapa yatafunguliwa kuanzia saa sita mchana

Kuwahi kwako uwanjani ndio tiketi yako kwani uwanja utakapokuwa umejaa, mageti yatafungwa!


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.