Baba yake Ansu Fati amjia juu Xavi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th March 2023


Baba yake Ansu Fati amjia juu Xavi

Bori Fati ni baba mzazi wa mshambuliaji wa FC Barcelona Ansu Fati ambaye tangu arejee kutoka kwenye majeraha amekuwa na wakati mgumu wa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza

Bori ameeleza masikitiko yake kwa kijana wake kutoaminiwa na kocha Xavi Hernandez wakati alipokuwa majeruhi ni Barcelona walioharakisha kumrejesha uwanjani

"Barcelona ilipokuwa mbovu zaidi kuliko ilivyo sasa, walimlazimisha Ansu kurejea kutoka kwenye majeraha ili kucheza. Walikuwa wakimtaka Ansu awafurahishe tena watu"

"Lakini sasa yuko fiti 100% na yuko tayari, hakuna anayemtaka. Muulizeni Xavi kwa nini hamchezeshi Ansu? mimi sina jibu lolote. Xavi anataka Ansu afanye kazi kwa bidii, na yuko hivyo lakini hapati nafasi"

"Mimi kama baba najisikia kukatishwa tamaa sana, mimi sina la kufanya ila ninasema tu, Xavi mpe fursa Ansu acheze"

"Nimezungumza na Xavi mara kadhaa, ni mtu mzuri, amemsaidia sana Ansu kimbinu, lakini sijui kwanini hampi nafasi," Bori alinukuliwa na mtandao wa GOAL


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.