Simba - Raja

Simba yamaliza kinyonge makundi Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Apr 2023
Simba yamaliza kinyonge makundi Ligi ya Mabingwa

Usiku wa kuamkia leo Simba ilikamilisha hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika wakikubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Raja Casablanca katika mchezo uliopigwa uwanja wa Mohammed V nchini Morocco

Katika kipindi cha kwanza Simba ilionekana kucheza kwa nidhamu kubwa wakiwanyima Raja nafasi ya kuipenya kirahisi ngome yao

Hata hivyo wakati mchezo ukielekea mapumziko, safu ya ulinzi ya Simba ilipoteza umakini wake ikawa rahisi kwa Khabba kuiandikia Raja bao la kuongoza kwenye dakika ya 44 baada ya kumzidi ujanja mlinzi wa Simba Joash Onyango

Kwenye kipindi cha pili Simba walirejea tofauti na iliwachukua dakika tatu tu kusawazisha bao hilo kupitia kwa Jean Baleke ambaye aliweka mpira katia nyavu tupu baada ya makosa ya mlinda lango wa Raja aliyekuwa ametoka langoni

Kuingia kwa bao hilo ni kama kuliwaamsha Raja na kupeleka mashambulizi mfululizo katika lango la Simba

Dakika ya Joash Onyango tena akamfanyia madhambi Khabba ndani ya eneo la hatari na mwamuzi kuamuru pigo la penati

Khabba hakufanya ajizi akaifungia Raja bao la pili. Boulacsoul akaongeza la tatu kwenye dakika ya 86

Simba sasa inasubiri droo ya hatua ya robo fainali itakayopigwa April 05 huko Misri

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’