Mkufunzi wa Bayern Munich Thomas Tuchel amefichua jinsi kikao cha dakika tatu hadi tano na mabosi wa Chelsea kilivyopelekea apoteze ajira yake kunako klabu hiyo
Akizungumza na wanahabri jana kuelekea mechi yake ya kwanza kama kocha mpya wa Bayern Munich dhidi ya wapinzani wake na viongozi wa sasa wa Bundesliga Borussia Dortmund, Tuchel alifichua kwamba alifukuzwa na The Blues wakati wa mkutano wa muda mfupi
"Ilikuwa mshtuko, nilihisi, ajabu, wakati nilipoendesha gari hadi kituo cha mazoezi," alisema kocha aliyeiongoza Chelsea kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa na pia kubeba UEFA Super Cup na Kombe la Dunia la Vilabu la FIFA katika kipindi chake cha miezi 20
"Mkutano haukuwa wa kawaida na uligeuka kuwa mkutano mfupi sana. Ilikuwa 8am, au kitu, na ilidumu dakika tatu hadi tano. Pia sikupata nafasi ya kuzungumza zaidi"
"Uamuzi ulikuwa umefanywa na kwa kweli, ilikuwa mshtuko kwani nilikuwa na hisia kwamba niko mahali pazuri kwa wakati unaofaa"
"Niliamini naweza kufanya mambo makubwa na nilitamani kukaa muda mrefu zaidi"
Tuchel alisema alikuwa amejenga mahusiano mazuri na wafanyakazi katika uwanja wa mazoezi wa Chelsea wa Cobham na kufukuzwa kwake bado kunawaumiza



