Chelsea - Bayern Munich

Tuchel afichua alivyotimuliwa Chelsea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Apr 2023
Tuchel afichua alivyotimuliwa Chelsea

Mkufunzi wa Bayern Munich Thomas Tuchel amefichua jinsi kikao cha dakika tatu hadi tano na mabosi wa Chelsea kilivyopelekea apoteze ajira yake kunako klabu hiyo

Akizungumza na wanahabri jana kuelekea mechi yake ya kwanza kama kocha mpya wa Bayern Munich dhidi ya wapinzani wake na viongozi wa sasa wa Bundesliga Borussia Dortmund, Tuchel alifichua kwamba alifukuzwa na The Blues wakati wa mkutano wa muda mfupi

"Ilikuwa mshtuko, nilihisi, ajabu, wakati nilipoendesha gari hadi kituo cha mazoezi," alisema kocha aliyeiongoza Chelsea kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa na pia kubeba UEFA Super Cup na Kombe la Dunia la Vilabu la FIFA katika kipindi chake cha miezi 20

"Mkutano haukuwa wa kawaida na uligeuka kuwa mkutano mfupi sana. Ilikuwa 8am, au kitu, na ilidumu dakika tatu hadi tano. Pia sikupata nafasi ya kuzungumza zaidi"

"Uamuzi ulikuwa umefanywa na kwa kweli, ilikuwa mshtuko kwani nilikuwa na hisia kwamba niko mahali pazuri kwa wakati unaofaa"

"Niliamini naweza kufanya mambo makubwa na nilitamani kukaa muda mrefu zaidi"

Tuchel alisema alikuwa amejenga mahusiano mazuri na wafanyakazi katika uwanja wa mazoezi wa Chelsea wa Cobham na kufukuzwa kwake bado kunawaumiza

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
25m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’