Manchester City yaichapa Liverpool 4-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st April 2023


Manchester City yaichapa Liverpool 4-1

Manchester City imeweka hai matumaini katika mbio za kuwania ubingwa wa Premia baada ya kuichapa Liverpool mabao 4-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Etihad

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola alijua ni lazima ashinde mechi hiyo City waliingia dimbani wakiwa nyuma kwa tofauti ya alama nane dhidi ya vinara wa ligi Arsenal

Liverpool walitangulia kufunga bao la kuongoza kupitia kwa Mohamed Salah wakati Diogo Jota alipovunja mtego wa kuotea kabla ya kumtengenezea Salah kuuweka mpira kimiani.

City walirudi na moto na haikuchukua muda kabla ya kupata bao la kusawazisha kupitia kwa Julian Alvarez baada ya pasi murua kutoka kwa Jack Grealish

Mabao mengine ya Manchester City yalifungwa na Kevin de Bruyne, Grealish na Ilkay Gundogan wakihakikisha wanarejea kwenye mbio za ubingwa sasa wakitofautiana na Arsenal alama tano kabla ya mechi ambayo Arsenal wanakabiliana na Leeds United

Ni moja ya siku mbaya kwa Liverpool katika ligi kuu ya Premia msimu huu kwani ukiondoa bao walilofunga, hawakuwa na hatari yoyote kwenye lango la Man City


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.