Yanga

Nyota watatu Yanga, Nabi kuikosa TP Mazembe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Apr 2023
Nyota watatu Yanga, Nabi kuikosa TP Mazembe

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema wamekuwa na muda mzuri wa maandalizi kuelekea mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya TP Mazembe ambao utapigwa kesho Jumapili

Kaze amebainisha kuwa siku mbili za mazoezi walizopata Lubumbashi zinatosha kuwaweka tayari kwa mchezo huo ambao Yanga inahitaji kushinda

"Tumefanya mazoezi mazuri jana baada ya safari ndefu na pua leo tutapata nafasi ya kujiandaa vizuri na mchezo wa kesho"

"Wachezaji wote wako vizuri naamini tutakuwa na mchezo kesho," alisema Kaze

Akizungumzia kikosi chake, Kaze amesema wachezaji Djigui Diarra na Khalid Aucho wataukosa mchezo huo wakitumikia adhabu ya kadi tatu za njano

Lakini pia kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki hatakuwa sehemu ya mchezo baada ya kuchelewa kutua DR Congo kutokana na changamoto ya usafiri akitoka kwenye majukumu ya timu ya Taifa

Kocha Mkuu Nasreddine Nabi nae hakusafiri na timu DR Congo kutokana na matatizo ya kifamilia

"Kocha mkuu Nasreddine Nabi ataukosa mchezo wa kesho dhidi ya Mazembe kwa sababu za Kifamilia. Mchezo huu ni muhimu sana kwetu kwa sababu malengo yetu ni kuwa vinara kwenye hatua hii ya Makundi"

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’