Yanga yaizamisha TP Mazembe Lubumbashi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd April 2023


Yanga yaizamisha TP Mazembe Lubumbashi

Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa kombe la Shirikisho uliopigwa uwanja wa TP Mazembe huko Lubumbashi, DR Congo

Bao la Farid Mussa lililopatikana kwenye kipindi cha pili lilitosha kuihakikishia Yanga ushindi huo muhimu ambao unaweza kuwahakikishia kumaliza vinara wa kundi D

Krosi ya Jesus Moloko ilimshinda mlinda lango wa Mazembe kabla ya kuangukia mguuni kwa Farid aliyeujaza mpira kimiani kwa mguu wake wa kulia

Ilikuwa mechi ngumu iliyopigwa katika uwanja wa nyasi bandia ambao kwa kiasi kikubwa uliwapa wakati mgumu wachezaji wa Yanga huku wenyeji wakitawala

Yanga imefikisha alama 13 wakati US Monastir wana alama 10 wakitarajiwa kucheza na Real Bamako saa 4 usiku

Ili kuishusha Yanga kileleni, Monastir watahitaji kushinda kuanzia mabao matatu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.