Azam - Mtibwa - Local

Azam Fc kuikabili Mtibwa Sugar robo fainali FA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Apr 2023
Azam Fc kuikabili Mtibwa Sugar robo fainali FA

Licha ya kuyumba kidogo tofauti na walivyoanza msimu huu kwenye ligi kuu, Azam Fc leo wana nafasi ya kufanya vizuri katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Mtibwa Sugar

Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi saa 1 usiku

Kwa Azam Fc kombe la FA sasa ni muhimu zaidi kwao ili kujihakikishia kushiriki michuano ya CAF msimu ujao

Kwenye Ligi Kuu wanashika nafasi ya nne nyuma ya Yanga, Simba na Singida Big Stars

Msimu ujao Tanzania itatoa timu nne kwenye michuano ya CAF ambapo mshindi wa kwanza na pili katika ligi kuu watacheza ligi ya mabingwa wakati mshindi wa tatu na bingwa wa kombe la FA watacheza kombe la Shirikisho

Kama itatokea bingwa wa FA ni timu iliyomaliza nafasi ya kwanza au pili kwenye ligi kuu, timu itakayoshika nafasi ya nne kwenye ligi itakwenda Shirikisho

Azam Fc wanakutana na Mtibwa Sugar ambayo msimu huu imekuwa haitabiriki. Timu hizo zilipokutana kwenye ligi uwanja wa Manungu, Azam Fc iliibuka na ushindi wa mabao 4-3

Baada ya mechi ya FA, timu hizo zitachuana tena katika mchezo wa ligi kuu utakaopigwa hapohapo kwenye uwanja wa Azam Complex, April 15

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
27m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’