Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne, April 04 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Apr 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne, April 04 2023

Graham Potter amekataa fursa ya kuchukua usukani kama meneja wa Leicester baada ya kutimuliwa Chelsea.(Talksport)

Potter atasubiri hadi msimu ujao kabla ya kuchukua kazi yake ijayo. (Mail) Meneja wa zamani wa Barcelona na Uhispania Luis Enrique ameibuka kama mtangulizi wa kuwa meneja mpya wa Chelsea. (Sun)

Chelsea wanataka kuwahoji mameneja watano kuhusu nafasi yao iliyo wazi, wakiwemo Enrique, Julian Nagelsmann, Mauricio Pochettino, Luciano Spalletti wa Napoli na mwingine mmoja. (Telegraph - subscription required)

Meneja wa Manchester United Erik ten Hag anaona nahodha wa Uingereza Harry Kane kama chaguo lake la kwanza la mshambuliaji msimu huu lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 yuko tayari kusajiliwa katika mkataba mpya Tottenham. (Athletic - subscription required)

Meneja wa Sporting Lisbon Ruben Amorim na bosi wa Eintracht Frankfurt Oliver Glasner pia wanazingatiwa. (Guardian)

Uongozi wa Chelsea una wasiwasi kuhusu umri wa mkufunzi wa zamani wa Bayern Munich Nagelsmann mwenye umri wa miaka 35. (Sky Sports)

Beki wa Uingereza Harry Maguire, 30, atauzwa United msimu huu huku Ten Hag akitoa wito kwa klabu hiyo kuwa na jeuri zaidi katika kukiondoa kikosini. (Manchester Evening News)

Manchester United wamefanya mazungumzo ya kiuchunguzi kuhusu kumsajili beki wa pembeni wa Ufaransa Benjamin Pavard, 27, kutoka Bayern Munich. (Athletic - subscription required)

United wameanza mazungumzo juu ya kumsajili beki wa pembeni wa Bayer Leverkusen na Uholanzi Jeremie Frimpong, 22. (Florian Plettenberg)

Tottenham watatafuta maoni ya Brendan Rodgers kuhusu kuwa meneja wao mpya kufuatia kutimuliwa kwake Leicester. (Football Insider)

Arsenal wamefanya mazungumzo na kiungo wa kati wa Ubelgiji Youri Tielemans, 25, ambaye mkataba wake na Leicester unakamilika msimu huu. (TeamTalk) Klabu ya Saudi Arabia ina nia kubwa ya kumnunua mshambuliaji wa Aston Villa na Brazil Philippe Coutinho, 30. (Football Insider)

Newcastle United ni mojawapo ya vilabu kadhaa vya Ligi ya Premia vinavyoonyesha nia ya kumnunua kiungo wa kati wa Manchester City, Muingereza Taylor Harwood-Bellis, 21, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Burnley. (90min)

The Blues wameongeza nia yao ya kutaka kumnunua mshambuliaji wa Atalanta na Denmark Rasmus Hojlund, 20. (Mail)

Chelsea wana makubaliano ya mdomo kumsaini kiungo wa Ecuador Kendry Paez, 15, kutoka Independiente del Valle katika mkataba ambao unaweza kuwa na thamani ya zaidi ya £17.5m. (Standard)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’