Okrah aiwahi Ihefu Fc

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th April 2023


Okrah aiwahi Ihefu Fc

Klabu ya Simba imethibitisha kurejea kikosini kwa kiungo mshambuliaji Augustine Okrah ambaye alikuwa nje kwa zaidi ya wiki nne baada ya kuvunjika kidole

Taarifa iliyotolewa na Simba, imebainisha kuwa leo Okrah ameshiriki mazoezi na wachezaji wengine kikamilifu

Aidha winga Kibu Denis nae afya yake imeimarika leo amejumuika na wenzake katika mazoezi

Kibu na Shomari Kapombe waliumia kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca uliopigwa Jumamosi iliyopita

Simba imeingia kambini kujiandaa na mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Ihefu Fc ambao utapigwa Ijumaa, April 07 katika uwanja wa Uhuru


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.