Simba - Local

Tutafanya maajabu robo fainali - Robertinho

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Apr 2023
Tutafanya maajabu robo fainali - Robertinho

Droo ya Robo Fainali ya mashindano ya CAF 2022/23, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho Afrika inatarajiwa kufanyika leo Jumatano, Aprili 5, 2023 mjini Cairo, Misri kuanzia saa 03:30 usiku

Droo hiyo itaonyeshwa moja kwa moja kwenye majukwaa ya kidijitali ya CAF na TV washirika. Wakati wadau wa soka nchini wakisubiri kwa hamu droo hiyo ili kujua wapinzani wa Simba na Yanga, Mkufunzi wa Simba Robertinho Oliveira ameanza maandalizi ya kikosi chake malengo ya Simba yakiwa kutinga nusu fainali

Lakini kabla ya mechi hizo za robo fainali CAF zitakazopigwa April 22-28, Simba inakabiliwa na mechi tatu muhimu ambapo moja ya robo fainali kombe la FA dhidi ya Ihefu Fc itakayopigwa Ijumaa April 07, mechi ya ligi kuu dhidi ya Ihefu Fc itakayopigwa April 10 na mechi ya ligi kuu dhidi ya Yanga itakayopigwa Apripl 16

Robertinho amesema kwa sasa wanajiandaa kwa mechi zinazofuata mbele lakini hawana hofu yoyote kwenye michuano ya ligi ya mabingwa kwani watakuwa tayari kupambana na timu yoyote watakayopangiwa

"Hatuwezi kuchagua mpinzani wa kukutana naye, yeyote ambaye tutapangwa naye tutakabiliana naye, tunaweza kufanya maajabu na kushangaza Afrika, tutafanya maandalizi hatua kwa hatua, yapo ambayo tuliyaona kwenye makundi tutadili nayo ili kuweka sawa mambo kabla ya hatua ya robo fainali"

"Siku zote nimekuwa na mtazamo chanya hivyo matarajio yangu ni makubwa, yaliyopita yamepita na kazi kubwa ni kuona vile ambavyo tunaweza kuwa bora maradufu hatua inayofuata, tupo pazuri nafikiri mashabiki wasubiri timu bora zaidi robo fainali"

"Tumeshafanya kazi ya kurekebisha makosa na muda tulionao tutamalizia, naamini kwenye ubora wa timu na hilo litatimia," alisema Robertinho

Simba itachuana na Mamelodi Sundowns, Esperance au Wydad Athletic katika hatua ya robo fainali ambapo mpinzani wake atafahamika baada ya droo itakayofanyika leo

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
30m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
42m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’