Simba - Local

Simba yaipania Ihefu Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Apr 2023
Simba yaipania Ihefu Fc

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Ihefu Fc ambao utapigwa Ijumaa, April 07 kwenye uwanja wa Azam Complex

Robertinho amesema anatambua mchezo huo hautakuwa mwepesi kwane wanakwenda kuchuana na timu iliyoimarika ambayo imetoa ushindani kwa timu zilizojuu kwenye msimamo wa ligi

"Hautakuwa mchezo rahisi lakini tunahitaji kucheza vizuri na kupata ushindi ili tusonge mbele hatua ya nusu fainali. Tunajua tunakwenda kukutana na timu ngumu lakini tumejipanga kuhakikisha tunashinda mchezo huo ili kutimiza malengo yetu," alisema Robertinho

Ihefu Fc tayari iko jijini Dar es salaam kuelekea mchezo huo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali

Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana kwenye ligi katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0

Baada ya mchezo wa kombe la FA, timu hizo zitaelekea Mbarali Mbeya kwa ajili ya mchezo wa duru ya pili ligi kuu ambapo utapigwa April 10 katika uwanja wa Highland Estates

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’