Lampard aanza kuinoa Chelsea

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th April 2023


Lampard aanza kuinoa Chelsea

Jana Chelsea walithibitisha kurejea kwa Frank Lampard kama kocha wa muda

Gwiji huyo wa Stamford Bridge amerejea na The Blues baada ya kutimuliwa kwa Graham Potter zaidi ya miaka miwili tangu yeye mwenyewe atimuliwe kama meneja

Lampard (44) alianza majukumu yake siku jana Alhamisi na atakuwa dimbani Jumamosi dhidi ya Wolves

Wamiliki wa pamoja wa Chelsea Todd Boehly na Behdad Eghbali walisema katika taarifa:

"Tuna furaha kumkaribisha Frank tena Stamford Bridge. Frank ni maarufu kwenye Premier League na gwiji katika klabu hii"

"Tunapoendelea na mchakato wa kusaka mkuu wa kudumu, tunataka kuipa klabu na mashabiki wetu mpango ulio wazi na thabiti kwa muda uliosalia wa msimu"

"Tunataka kujipa kila nafasi ya kufaulu na Frank ana sifa zote tunazohitaji ili kutufikisha kwenye mstari wa kumalizia"

"Tuna mchezo muhimu dhidi ya Wolves Jumamosi na kisha tutaelekeza mawazo yetu kwenye robo fainali ya Ligi ya Mabingwa huko Madrid wiki ijayo. Sote tutampa Frank msaada wetu kamili tunapolenga kupata matokeo bora kutoka kwa michezo yetu yote iliyosalia"


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.