Timu ya wasichana ya shule ya sekondari ya Fountain Gate Dodoma, imeibuka mabingwa wa mashindano ya soka ya shule za Afrika ya CAF
Ni baada ya ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wa fainali dhidi ya Ecole Omar Ibn Khatab ya Morocco huko Afrika Kusini
Mashindano hayo yaliokuwa yanawakutanisha mabingwa wa kanda za Afrika kwa Wavulana na Wasichana, yamefanyika mjini Durban nchini Afrika Kusini na yalianza katikati mwa wiki hii
Haya ni mafanikio makubwa zaidi kwa timu hiyo, ambayo ilipata nafasi baada ya kuibuka mabingwa wa mashindano hayo katika Kanda ya Afrika Mashariki na kati (Cecafa).



