Fountain Gate yashinda mashindano ya shule Afrika

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th April 2023


Fountain Gate yashinda mashindano ya shule Afrika

Timu ya wasichana ya shule ya sekondari ya Fountain Gate Dodoma, imeibuka mabingwa wa mashindano ya soka ya shule za Afrika ya CAF

Ni baada ya ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wa fainali dhidi ya Ecole Omar Ibn Khatab ya Morocco huko Afrika Kusini

Mashindano hayo yaliokuwa yanawakutanisha mabingwa wa kanda za Afrika kwa Wavulana na Wasichana, yamefanyika mjini Durban nchini Afrika Kusini na yalianza katikati mwa wiki hii

Haya ni mafanikio makubwa zaidi kwa timu hiyo, ambayo ilipata nafasi baada ya kuibuka mabingwa wa mashindano hayo katika Kanda ya Afrika Mashariki na kati (Cecafa).


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.