Erling Haaland amefikia rekodi nyingine ya Premier League kwa kupachika mabao mawili dhidi ya Southampton katika ushindi wa 4-1
Manchester City sasa wako nyuma ya Arsenal kwa pointi tano baada ya kupata ushindi muhimu dhidi ya timu ya Ruben Selles kwenye Uwanja wa St Mary's
Haaland aling'ara tena akifunga bao lake la kwanza kwa kuunganisha kwa kichwa krosi ya Kevin De Bruyne kabla ya kwenda mapumziko, ambayo ilikuwa assist ya 100 ya Mbelgiji huyo kwenye Ligi Kuu ya Uingereza.
Nyota huyo wa zamani wa Chelsea akatengeneza asisti nyingine kwa Jack Grealish, ambaye aliendeleza kiwango chake kizuri kwa bao lingine wikendi hii.
De Bruyne amefikisha assist 10 kwa muda wa haraka zaidi kwa mchezaji wa Premier League, amefanya hivyo katika mechi 237.
Mchezaji anayeshika nafasi ya pili ni Cesc Fabregas, alichukua mechi 298 na kupata asisti 100. Dakika chache kabla ya bao la kwanza la City, Haaland alikuwa amekosa nafasi nzuri kabla hajafunga bao la mechi ambalo ni la 43 la msimu katika mashindano yote
