Juventus - Inter Milan - International

Ubaguzi kwa Lukaku waiponza Juventus

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Apr 2023
Ubaguzi kwa Lukaku waiponza Juventus

Klabu ya Juventus imepewa adhabu ya kucheza mchezo mmoja bila sehemu ya jukwaa moja la mashabiki wao baada ya kumtusi kwa kejeli za kibaguzi mshambuliaji wa Inter Milan, Romelu Lukaku

Lukaku alilengwa na mashabiki wa Juventus kabla na baada ya kufunga penati dakika ya tano ya muda ulioongezwa na kuwafanya Inter kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya mkondo wa kwanza ya nusu fainali ya Coppa Italia iliyochezwa Jumanne iliyopita

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji alipewa kadi ya pili ya njano kwa kuweka vidole kwenye midomo yake ili kuwanyamazisha mashabiki kwenye Uwanja wa Allianz

Bodi ya Ligi Kuu Italia, Serie A, imetangaza Juve lazima wafunge jukwaa moja la Kusini kwa mchezo wao ujao wa ligi ya nyumbani, ambao ni dhidi ya Napoli utakaochezwa Aprili 23, mwaka huu

Lukaku bado atatumikia adhabu ya kufungiwa mechi moja katika mechi ya marudiano na Juve itakayochezwa Aprili 26, mwaka huu kwa kuonyeshwa kazi nyekundu.

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
25m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’