Simba - Local

Simba yaiduwaza Ihefu Fc Mbarali

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
10 Apr 2023
Simba yaiduwaza Ihefu Fc Mbarali

Wanasema mfupa uliwashinda wengi umelika kilaini leo na Mnyama Simba!

Ni baada ya Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ihefu Fc katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Highland Estates, Mbarali Mbeya

Kabla ya kipigo cha leo, Ihefu hawakuwa wamepoteza mchezo katika uwanja wao wa nyumbani dhidi ya timu kutoka jijini Dar es salaam

Yanga, KMC na Azam Fc zote zilichezea kichapo katika dimba la Ihefu

Hata hivyo mabao mawili ya mshambuliaji hatari wa Simba Jean Baleke yalitosha kuihakikishia alama tatu muhimu katika mchezo mgumu

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake akiwaacha nje nyota wake muhimu

Mabadiliko hayo yaliibua lawama miongoni mwa mashabiki wa Simba kabla ya mchezo 

Lakini Robertinho ameibuka shujaa baada ya dakika 90 timu yake ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0

Ni ushindi ambao unaifanya Simba iendelee kuweka hai matumaini katika mbio za ubingwa wakifikisha alama 60 alama tano nyuma ya vinara wa ligi Yanga wenye alama 65

Yanga itacheza na Kagera Sugar katika uwanja wa Azam Complex siku ya Jumanne

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
31m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
43m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’