Yanga - Kagera - Local

Yanga yaifumua Kagera Sugar 5-0

Joel JJ By Joel JJ
11 Apr 2023
Yanga yaifumua Kagera Sugar 5-0

Yanga inazidi kuukaribia ubingwa wa 29 Ligi Kuu ya NBC baada ya kuifumua Kagera Sugar mabao 5-0 katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Stephane Aziz Ki alikuwa shujaa wa Yanga katika mchezo huo akifunga mabao matatu 'hat-trik', mawili yakiwa mikwaju ya penati na moja likiwa bao la 'kideo' akiwa umbali takribani mita 25

Dhamira ya ushindi kwa Yanga ilionekana mapema kwenye kipindi cha kwanza, Fiston Mayele alikuwa na uchu wa kuongeza mabao yake

Alifanikiwa kufunga bao kwenye kipindi cha pili baada ya kosakosa nyingi katika kipindi cha kwanza

Bernard Morrison nae amerejea na bao lake, akiweka kambani bao la nne kwa shuti kali akiwa nje kidogo ya 18

Ilikuwa mechi ambayo Yanga walitawala na pengine walistahili kufunga zaidi ya mabao matano

Mayele amejiimarisha kileleni katika mbio za ufungaji bora akifikisha mabao 16, idadi sawa ya mabao ambayo alifunga msimu uliopita

Mabao yake matatu aliyofunga Aziz Ki leo, yamemfanya afikishe mabao nane msimu huu wakati Morrison amefunga bao lake la tatu leo

Yanga imerejesha gap la pointi nane dhidi ya watani zao Simba baada ya kufikisha alama 68 kileleni mwa msimamo wa ligi

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
3h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
6h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
6h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
7h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
7h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
7h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
7h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
8h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →