Lukaku afunga Inter ikiichapa Benfica 2-0 UEFA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th April 2023


Lukaku afunga Inter ikiichapa Benfica 2-0 UEFA

Inter Milan walitumia dakika 45 za kipindi cha pili kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya benfica na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya

Nico Barella na Romelu Lukaku walifunga mabao hayo yanayowaweka mbele Inter kuelekea mechi ya mkondo wa pili utakaopigwa Italia wiki ijayo

Barella alifunga kwa kichwa katika dakika ya 51, akimalizia krosi nzuri kutoka kwa beki wa kati Alessandro Bastoni, ambaye alikuwa akishambulia upande wa kushoto

Lukaku aliyetokea benchi, alifunga penalti dakika ya 82 baada ya VAR kuelekeza mpira uliogonga mkono wa nahodha wa Benfica Joao Mario 

Mabao hayo mawili yanaipa Inter faida kubwa katika mchezo wa marudiano utakaopigwa San Siro Jumatano ijayo, ambapo watakuwa na nafasi kubwa ya kutinga nusu-fainali ya Italia dhidi ya majirani zao AC Milan au Napoli


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.