Inter Milan walitumia dakika 45 za kipindi cha pili kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya benfica na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya
Nico Barella na Romelu Lukaku walifunga mabao hayo yanayowaweka mbele Inter kuelekea mechi ya mkondo wa pili utakaopigwa Italia wiki ijayo
Barella alifunga kwa kichwa katika dakika ya 51, akimalizia krosi nzuri kutoka kwa beki wa kati Alessandro Bastoni, ambaye alikuwa akishambulia upande wa kushoto
Lukaku aliyetokea benchi, alifunga penalti dakika ya 82 baada ya VAR kuelekeza mpira uliogonga mkono wa nahodha wa Benfica Joao Mario
Mabao hayo mawili yanaipa Inter faida kubwa katika mchezo wa marudiano utakaopigwa San Siro Jumatano ijayo, ambapo watakuwa na nafasi kubwa ya kutinga nusu-fainali ya Italia dhidi ya majirani zao AC Milan au Napoli



