Sugu ajitosa kuinusuru Mbeya City

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th April 2023


Sugu ajitosa kuinusuru Mbeya City

Aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini (2010-2020), Joseph Osmund Mbilinyi 'Sugu' ameahidi Kutoa Milioni Moja Kwa kila Goli litakalo fungwa na Mbeya City

Sugu amebainisha kuwa anafanya hivi ili kuipa hamasa timu hiyo isishuke Daraja

"Mbeya City Stand Up!! Timu yetu iko hatarini kushuka daraja, TUSIKUBALI! Tumebakiza mechi 4 na ili kupona inabidi tushinde hata mechi 2 tu. Katika kuhamasisha Wachezaji uwanjani, nitatoa 1M kwa kila GOLI la USHINDI kwa mechi zilizobaki na mkwanja utaenda kwa mfungaji, " Sugu aliandika kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii

Mbeya City inashika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC ikiwa kwenye eneo la play-off


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.