Kikosi cha Singida Big Stars kinarudi mazoezini leo Alhamisi kwa ajili ya kujiandaa na michezo mbalimbali lakini ndani ya siku 10 zijazo kitakuwa bila ya Kocha Mkuu Mholanzi, Hans Van Der Pluijm
Baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Polisi Tanzania katika mchezo wa ligi kuu April 07, mchezo unaofuata ni dhidi ya mabingwa watetezi Yanga ambao bado haujapangiwa tarehe ya TFF
Pluijm ameelekea Marekani kwa ajili ya kuhudhuria ndoa ya mwanaye huku Kocha Msaidizi wa timu hiyo Mathias Lule nae akiondoka baada ya kufiwa na Mama yake mzazi
Kikosi cha Singida BS kinajifua chini ya Mkurugenzi wa Ufundi, Ramadhan Nswanzurimo katika muda ambao makocha hao watakosekana
Singida BS inakabiliwa na mechi mbili dhidi ya Yanga kwani baada ya mchezo wa ligi, timu hizo zitakutana kwenye mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) mechi zote zikipigwa uwanja wa Liti