Manchester City wanazidisha joto kwa Arsenal katika mbio za kuwania taji la Ligi ya Premia huku vijana wa Pep Guardiola wakilenga ushindi wa 10 mfululizo wakati Leicester watakapozuru Etihad Jumamosi.
Uongozi wa Arsenal kwa pointi sita kileleni mwa jedwali unaweza kupunguzwa kwa nusu kabla hawajazuru West Ham Jumapili
Mechi zote mbili pia zitakuwa na athari kwa wapinzani wao katika vita ya kujinusuru kushuka daraja wakiwa na pointi sita pekee zinazowatenganisha Leicester katika nafasi ya 19 kutoka kwa Wolves katika nafasi ya 13
Aston Villa walio katika kiwango bora wanaweza kuingia katika kinyang'anyiro cha nne-bora wakati Newcastle walio nafasi ya tatu watakapotembelea Villa Park.
Manchester United pia wanatazamia kupiga hatua karibu na Ligi ya Mabingwa msimu ujao huko Nottingham Forest



