Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi April 15 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Apr 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumamosi April 15 2023

Chelsea wako tayari kumfanya kiungo wa kati wa Barcelona na Uhispania Gavi kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa pesa nyingi kwenye Premier League ili kumsajili kinda huyo mwenye umri wa miaka 18. (AS - in Spanish)

The Blues pia wana imani kuwa wanaweza kushinda mbio za kumnunua mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, hata bila ya kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao. (90min)

Liverpool wamemfanya mchezaji wa kimataifa wa Argentina wa Brighton Alexis Mac Allister, 24, kuwa mlengwa wao mkuu kama kiungo wa kati msimu huu. (Football Insider)

Mshambulizi wa Crystal Palace na Ivory Coast Wilfried Zaha, 30, anatazamiwa kukataa kuhamia Saudi Arabia na kusalia Ulaya mara tu atakapokuwa mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu. (Evening Standard)

Mshambulizi wa Uingereza Harry Kane, 29, atasubiri kutathmini mkataba mpya katika klabu ya Tottenham mara tu klabu hiyo itakapomteua meneja mpya, huku Manchester United na Bayern Munich zikiwa na nia ya kumsajili. (90min)

Manchester City na Liverpool wanamtazama mlinzi wa Chelsea Mwingereza mwenye umri wa miaka 20 Levi Colwill, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Brighton. (Standard)

Mbali na Colwill, Liverpool pia wanavutiwa na viungo wa Chelsea wa Uingereza Conor Gallagher, 23, na Mason Mount, 24. (Football Insider) Lakini Chelsea wanatarajiwa kufanya msukumo wa mwisho kumshawishi Mount kusaini mkataba mpya. (ESPN)

The Blues wamefanya mazungumzo na Ruben Amorim wa Sporting Lisbon, 38, huku msako wa klabu hiyo wa kutafuta meneja mpya wa kudumu ukiendelea. (Guardian)

Barcelona wanakaribia kufikia makubaliano na nahodha wa Manchester City na kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 32. (90min) Manchester City ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia winga wa Portsmouth Koby Mottoh mwenye umri wa miaka 16. (Football Insider)

Chelsea inaweza kuuza wachezaji tisa wa kikosi cha kwanza ili kusawazisha fedha zao, huku mshambuliaji wa Marekani Christian Pulisic, 24, akiwa kati ya wale ambao wanaweza kuondoka. (Mirror)

Roma wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Brazil Roberto Firmino, 31, mkataba wake na Liverpool utakapokamilika msimu huu. (Nicolo Schira)

Roma pia wanafikiria kumsajili beki wa pembeni wa Leicester City na England James Justin, 25, kwa mkopo na chaguo la kufanya uhamisho huo kuwa wa kudumu kwa ada ya euro 20m (£17.7m). (Calciomercato - in Italian)

Liverpool ni miongoni mwa vilabu kadhaa vinavyomfuatilia winga wa Lyon na Ufaransa chini ya umri wa miaka 21 Bradley Barcola, 20. (Fabrizio Romano)

Fulham itaweka bei ya pauni milioni 60 kwa kiungo wa kati wa Ureno Joao Palhinha, 27, ambaye analengwa na Manchester United. (Metro)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’