Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dk Samia Suluhu Hassan ameipongeza klabu ya Simba kwa kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jana
Katika ujumbe wake alioweka kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii, Dk Samia amesema mchezo baina ya timu hizo watani unawakutanisha Watanzania wengi na kwa wakati mmoja na kuwapa burudani kwa namna ya kipekee
"Hongereni Simba kwa ushindi mliopata dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC. Upinzani wenu wa jadi uwanjani ni burudani inayowaleta pamoja mamilioni ya Watanzania kutoka katika kila kona ya nchi yetu, kwa namna ya kipekee," aliandika Dk Samia
Mabao ya Hennock Inonga na Kibu Denis ndio yaliyopeleka kilio Jangwani na kuwaacha watani wakiwa wamepigwa na butwaa baada ya kupelekewa pumzi ya moto kutoka kwa vijana wa Msimbazi!
Hongereni Simba kwa ushindi wenu dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Upinzani wenu wa jadi uwanjani ni burudani inayowaleta pamoja mamilioni ya Watanzania katika kila kona ya nchi yetu, kwa namna ya kipekee. #KariakooDerby pic.twitter.com/LAzxwwuKZu
β Samia Suluhu (@SuluhuSamia) April 16, 2023



